Nilipokaa kutahajudi wakati wa kipindi cha Neena kwenye Pasaka, dhamira yangu ilikuwa ni kukaa, na kama nikipata heri, kufikia initiation ya pili. Nilipokea initiation ya kwanza katikati ya Desemba iliyopita, na nimekuwa natahajudi kwa uaminifu kwenye ya Mwanga na Sauti tangu wakati huo. Sasa, hebu nitangulie kusema kwamba mimi si mgeni wa kutahajudi. Nilianzishwa kwenye Transcendental Meditation miaka 45 iliyopita, na nimetumia idadi ya mifumo mingi tangu wakati huo, ikiwa ni pamoja na njia moja pekee kwa muda wa miaka 20 iliyopita. Baadhi ya njia hizi zilinisaidia sana kiroho, na mimi milele nazishukuru kwa michango yao katika ukuaji wangu na utayari wa kiroho. Hata hivyo, hakuna hata mmoja ambayo ilinifikisha “huko.”
Enlightenment mara zote imekuwa lengo la maisha yangu, ingawa kuwa ni nini maana yake siku zote ilionekana kutokuwa wazi. Hivyo, nilipokaa wiki kadhaa zilizopita, sikuwa na uhakika nini kitatokea. Hata hivyo, mambo yalienda haraka, hasa baada ya mimi kuachia matarajio yangu. Nilianza kila tahajudi kwa kauli kwa Uongozi, “Nipo hapa. Fanyeni mnavyopenda” na kwa Neema, nilipata initiation ya pili tarehe 9 mwezi wa Aprili. Nikiwa nimehamaswa pamoja na kuihimizwa na kusaidiwa na baadhi ya Adepts (F), (D), (N), na (M), Niliongeza maradufu azimio langu la kukaa, na kujiachia kuwa wazi, na kuruhusu. Ni muhimu kwangu kusema hapa kwamba siku”fanya” kitu chochote katika mchakato huu. Kwa maneno mengine, mimi nilikuja tu, na kujitoa kwa Uongozi na Neema ya Mungu. Siku tatu baadaye, tarehe 12 Aprili, kwa njia ya muujiza wa kweli wa Neema hii, mimi kufikia Enlightenment yangu.
Sijawahi kuwa na uzoefu wa kitu kama tukio la Enlightenment katika miaka yangu yote ya kutahajudi. Nilisafirishwa na kuwa mahali penye ukimya, utulivu na amani. Nikawa hakuna (sio kitu) na kila kitu. Tofauti zote zikatatuliwa. Nilikuwa na amani, amani ambayo ilipita ufahamu wote. Hapa ni lazima kuomba msamaha, kwani ninapojaribu, maneno yanashindwa kuelezea hali hii. Hata hivyo, ni kuwa haisahauliki. Na sio kwamba mimi nakumbuka, ila mimi ni hiyo Hali.
Sasa mimi nina amani, ingawaje niko kwenye hekaheka duniani. Sina tena majadiliano ya mawazo ya akili inayo kimbiakimbia. Akili yangu imetulia kimya kabisa labda kama nataka kufikiria kitu. Ninapomaliza kufikiria, mawazo yanatoweka. Tabia ya mtazamo wangu wa kuwahukumu wengine imetoweka, na nafasi yake imechukuliwa na hisia na ufahamu wa uhusiano. Hisia za furaha zinashikilia shughuli zangu za kawaida, na naelewa kwamba jambo muhimu sana la kweli, ni UPENDO, unaojionyesha kwa njia ya wema na huduma.
Ni kwa shukrani kubwa basi, kwamba nashukuru Mwanga na Sauti, Uongozi wa Kiroho, na Adepts kwa kunipa kwa miezi nne kile ambacho sikupata miaka 45 iliyopita, zawadi ya Neema safi, ya Enlightenment.