Ushuhuda (S.B.)

 


Kuanzishwa


Sauti ilisikika kichwani kwangu, ikazidi kuongezeka na nzuri kusikika na kuenea mwilini mwangu, na kuufanya mwili wangu kuwa na mtetemo ukifuatiwa na mwanga mkali.

Mara moja moyo wangu ukajazwa na furaha, wepesi na nguvu, seli zote mwilini mwangu zilitikisa Nishati hii nzuri.

Kisha nilikuwa nikivutwa kupitia turujiza la giza ambalo lilikuwa ghafla nyeusi sana kuliko nyeusi, haikuwa kitu hapo, hakuna yeyote, hakuna MIMI
na hiyo iliniogopesha kidogo, Ufahamu safi tu

Kisha nikarudi kwenye Mwanga ambao ilikuwa na nguvu sana na wa kung’aa moyoni mwangu na kulipuka kwa nguvu kubwa ambayo ilinivuta wima kwenda juu. Nilihisi kama nilikuwa nikichukuliwa kwenda juu.

Niliona kupaa kwangu kwa upitishaji. Na pia niligundua ni mifumo gani katika maisha yangu ambayo mimi huchagua mara nyingi, kuzuia kupaa. Baada ya kufahamu haya, kupaa kwangu kulikuwa kwa kiasili na rahisi, ilitokea tu. Nilijihisi kama unyoya nikipanda kwa urahisi.

Ghafla niligundua Utatu katika Mwangaza mzuri.

Na nilichukukuliwa katika hali ya kina ya kutahajudi zaidi.

Hapakuwa na Mwangaza wowote tena bali utambuzi tu kuwa sio lazima kufanya kitu chochote, kwamba hunitahajudi kila wakati na kwa hivyo hakuna juhudi.

Nilipoteza hisia za nafasi na wakati na ghafla, nikaona picha yangu mwenyewe, nimesimama mbele ya Viumbe Wengi.

Nilikuwa na hakika kuwa nitakufa sasa. Kwa wakati mmoja Mwanga wa zambarau ulijaa papo hapo kwenye mwili wangu, Mwangaza ukawa na nguvu na wakati uliofuata sikuwa tena, nikatoweka na nilikkuwa, nafasi tupu ikabaki.

Nilihisi hali ya uhuru na kuamini (trust) wakati huo huo na kwamba kila kitu kilikuwa sawa kama kilivyo!